Somo
la leo tarehe 27/04/2020
Na
Mwl.
Isaack Manase Mtalambilwa
Simu:
0768 740 225
Dodoma
mjini.
Mada:
KAMUSI
KAMUSI YA LUGHA; MAANA,
AINA, TAARIFA NA DHIMA ZAKE.
MAANA YA KAMUSI
Massamba (2012:24)
kamusi ni kitabu cha orodha ya maneno katika lugha, yaliyopangwa kwa utaratibu
maalum, pamoja na maana au fasili zake; katika uchanganuzi wa lugha haya ni
maneno ya kileksika, yaani yasiyokuwa ya kisarufi au kifonolija.
Tuki (1990:21) kamusi
ni kitabu cha orodha ya maneno yaliyopangwa kwa utaratibu maalum, pamoja na
maana na fasili zake.
Wamitila (2003:76)
kamusi ni kitabu ambacho kina orodha ya maneno katika lugha Fulani ana ambayo
hupangwa ki-abjadi au kialfabeti. Maneno haya huelezewa maana zake mbalimbali
na labda hata vyanzo vyake.
Kwa ujumla kamusi ni kitabu chenye orodha ya maneno
mbalimbali yaliyopangwa vizuri kwa kufuata alfabeti na hutoa taarifa mbalimbali
kama vile maana, matamshi n.k.
MUUNDO WA KAMUSI
i) Utangulizi wa Kamusi
Hii ni sehemu ya mwanzo
ambayo hutangulia matini yenyewe ya kamusi.
ii) Matini ya Kamusi
Hii ni sehemu ambayo
inaonyesha vidahizo na fahiwa zake kuanzia herufi A-Z.
iii) Sherehe ya Kamusi
hizi ni baadhi ya
taarifa ambazo huwa zimeandikwa mwishoni mwa kamusi. Kwa mfano majina ya nchi,
lugha za mataifa duniani, vipimo vya urefu, vipimo vya uzito, ujazo n.k.
AINA ZA KAMUSI
Kwa kutumia kigezo cha
LUGHA kuna aina kuu tatu (3) za kamusi
i) kamusi wahidiya
hii ni kamusi
inayoandikwa kwa lugha moja
ii) kamusi thaniya
Hii ni kamusi
inayoandikwa kwa lugha mbili.
iii) kamusi mahuluti
Hii ni kamusi
inayoandikwa kwa lugha zaidi ya mbili. Kwa mfano
Kiswahili-kiingereza-kifaransa.
Taaarifa zinazopatikana
katika kamusi
Taarifa hizi huweza
kuwa za kisarufi au kileksika
a) taarifa za kisarufi
zinazoingizwa katika kamusi.
Nyambari na Masebo
(2012:184) wameainisha taarifa zifutazo za kisarufi zinazopatikana katika
kamusi.
• Wingi wa nomino
• Kategoria ya kisarufi ya kidahizo mf.
Kitenzi (kt), nomino (nm) n.k
• Vinyumbuo vya vitenzi mf.
Piga-pigwa-pigana-pigika n.k
• Ngeli za nomino mf. Mtu (A-YU), kazi
(i-)
• Matamshi ya neno
• Elekezi au sielekezi. Mfano: Apiza
kt [ele], Anguka kt [sie]
• Mifano ya matumizi
b) Taarifa za kileksia
zinazopatikana katika kamusi
• Mpangilio wa vidahizo
• Kategoria za maneno
• Umoja na wingi
• Upatanisho wa kisarufi
• Uelekezi wa vitenzi
• Maana ya vidahizo
• Tahajia za maneno
• Mifano ya matumizi
• Methali, nahau na misemo
• Timolojia ya leksimu
• Michoro/ picha
• Matamshi
DHIMA ZA KAMUSI
• Huonesha tahajia sahihi za maneno
• Huonesha maana za maneno
• Huonesha matamshi sahihi ya maneno
• Huonesha asili ya neno
• Humsaidia mtumiaji kujifunza lugha za
kigeni
• Huonesha alama na vifupisho mbalimbali
katika lugha husika.
KAZI YA KUFANYA
1. Taja faida 5 za kamusi.
Marejeleo
Massamba.
D.P.B.(2004 ). Kamusi ya isimu na falsafa ya lugha. Dares salaam: TUKI
TUKI
(1990).kamusi sanifu ya isimu na lugha. Dares salaam: Tuki na Educational
publishers and distributors ltd.
Wamitila.
K. W. (2003). Kamusi ya fasihi, istilahi na nadharia. Nairobi: Focus publishers
ltd.
CORONA
(COVID 19) INAUA: TUFATE USHAURI WA WATAALAMU NA SERIKALI KUJIKINGA
BAKI NYUMBANI, UBAKI SALAMA
No comments:
Post a Comment